Jux na Vanessa Mdee Hawalifichi Tena Penzi Lao, Jack Patrick Hana Chake

Jux na Vanessa Mdee hawataki tena kuficha uhusiano wao. Tangu mwaka mpya uanze, waimbaji hao wameuachia ulimwengu ufahamu kuwa ni wapenzi na wanapenda baada ya kipindi kirefu cha tetesi za uhusiano wao ambazo walikuwa wakizikanusha.
Uhusiano huo umepelekea hadi Jux amtumie Vee Money kama mpenzi wake kwenye video ya ‘Sisikii’ na kama umeitazama utakuwa umegundua chemistry ya kuvutia kati yao.
JUX
Weekend hii wawili hao wakiwa pamoja na Navy Kenzo, walikuwa na show visiwani Zanzibar ambapo Jux pamoja na kutumbuiza nyimbo zake, alipanda jukwaani kumpa kampani mpenzi wake huyo kwa kuchukua nafasi ya Barnaba wakati alipokuwa akitumbuiza wimbo ‘Siri’.
Baada ya show hiyo wapenzi hao walijumuika pamoja kula upepo kwenye beach za Zanzibar na mashabiki wao wanafurahia tu kuwaona pamoja.
Jack Patrick Kabla hajakamatwa na Madawa ya Kulevya Maccau Ndio alikuwa Mpenzi wa Jux , Akitoka Jala Atakuta Jux si wake Tena…..

0 comments:

 

LIKE PAGE YETU UWE WA KWANZA KUPATA HABARI MPYA. Just Click Like Button Below...

Powered By OnlineBlogger