Jokate Amzawadia KANDAMBILI Wema Sepetu

Mbunifu wa mavazi na mtangazaji Bongo, Jokate Mwegelo amesababisha shosti yake, Wema Sepetu ‘Madam’ afurahi baada ya kumpelekea zawadi ya kandambili zake za Kidoti pamoja na vipodozi mbalimbali.
kidoti
 
Jokate alisema Wema ni miongoni mwa watu ambao anawakubali kutokana na mchango mkubwa katika tasnia ya filamu Bongo, hivyo ameamua kumpelekea zawadi  ya bidhaa zake za Kidoti kuonesha heshima yake.
 
“Zawadi zangu niliwapa watu mbalimbali mmoja wapo akiwa ni shoga yangu wa kitambo Wema, hii inaonyesha ni jinsi gani nina mapenzi makubwa kwake,” alisema Jokate.  
 
Kwa upande wake Wema, alifurahi na kusema amependa zawadi hiyo anamuomba Mungu azidi kumfungulia milango Jokate katika bidhaa zake mbalimbali anazosa-mbaza.

0 comments:

 

LIKE PAGE YETU UWE WA KWANZA KUPATA HABARI MPYA. Just Click Like Button Below...

Powered By OnlineBlogger