Wakati
mkongwe wa filamu za kuchekesha, King Majuto akidai kutoshiriki kazi na
msanii yeyote kutokana na kuibiwa, msanii mwenzake, Aunty Ezekiel
amechukizwa na uamuzi huo.
Akizungumza
na Uwazi, Aunty alisema kuwa haamini kama wezi wa kazi zake ndiyo
chanzo cha Majuto kuachana na filamu za kushirikishwa bali inawezekana
kuna tatizo lake lingine.
“Suala
la wezi lipo miaka mingi na kama mkongwe na mpenda maendeleo alitakiwa
kusimama maana kila mmoja akisema achukue uamuzi kama huo ni wazi kwamba
kutakuwa hakuna msanii tena Tanzania,” alisema.
0 comments:
Post a Comment