Umuhimu na Jinsi ya Kutunza Majina na Namba za Simu Kwenye Kompyuta

Imekuwa ni tatizo kwa wengi kupoteza kumbukumbu muhimu katika simu kama vile anuani na majina ya watu katika simu za mkononi.
Utasikia mtu akisema kwenye simu “wewe nani? Sina namba yako kwa sababu simu yangu ilipotea na nikapoteza namba zote”.
Ukweli ni kwamba simu nyingi za kisasa zinauwezo wa kutunza namba za simu kwenye kompyuta  pamoja na taarifa nyingine kama picha,muziki na sms kama faili ambazo unaweza ukazisoma kupitia kompyuta; au ukarudishia kwenye simu pale unapopoteza simu au kufuta taarifa kwenye simu yako.

Njia ya Kwanza: Kutumia Bluetooth
mawasiliano-simu-kompyuta
Bluetooth ni teknolojia ya kuunganisha vifaa viwili vya kielectroniki kuwasiliana na kutuma na kupokea taarifa. Inaweza ikawa mafaili ya muziki,picha,video na hata namba za zimu au anuani.
Mawasiliano yanaweza kuwa kati ya kompyuta na simu au simu na simu.
Unaweza kutumia njia hii kutuma namba za simu na anuani toka kwenye simu yako na kuhifadhi kwenye kompyuta na ukaweza kurudisha tena katika simu yoyote nyingine toka kwenye kompyuta.
Sharti ni kuwa vifaa vyote viwili vinatakiwa kuwa na teknologia hiyo ya bluetooth

Njia ya Pili: Kutumia Waya Maalumu wa USB
bluetooth-connection-phone-pc
Waya wa USB unaweza kuunganisha simu yako ili kuwasiliana na kompyuta. Kwa kutumia program maalumu ambazo simu nyingi huja nazo utaweza kuunganisha kompyuta yako na simu. Programu hizi zinakuwezesha kufanya mambo mengi kama vile unavyoweza kufanya kwenye simu ila sasa kwa kutumia kompyuta.
Mfano unaweza kutuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) na hata kupiga simu na kuongea kama kompyuta yako ina mic na spika.
Kwa kutumia programu za aina hii unaweza ukapakua majina na hata taarifa nyingine kama  SMS na picha toka kwenye simu na kuweka kwenye kompyuta na kurudisha tena kwenye simu pale inapohitajika.

Njia ya Tatu: Kutunza Taarifa Kwenye Hifadhi ya Intaneti
cloudstore-connection-phone
Ukiwa na simu aina ya Smartphone na umeunganishwa kwenye mtandao wa intaneti,unaweza ukahifadhi kumbukumbu za simu yako ikiwemo majina na namba za simu kwenye hifadhi za intaneti (“Cloud Storage”) mfano wa huduma hizo ni ile inayotolewa na Google iitwayo Google Drive , Dropbox ,skydrive (Sasa inaitwa OneDrive) na nyingine nyingi.
Unaweza ukajiunga moja kwa moja toka kwenye simu au kutumia kompyuta.
Kama unatumia kompyuta unaweza ukajiunga na huduma hizi na kutumia kama diski ya kawaida katika kompyuta yako.

Njia ya Nne: Kupakua kwenye Kadi ya Kumbukumbu ya Simu (Memory Card)
sd-card-storage
Unaweza ukahamisha majina yote kwenda kwenye faili katika kadi ya simu.
Kisha ukahamisha faili toka kwenye kadi ya simu kwenda kwenye kompyuta kutumia blutooth au waya wa USB.
Pia unaweza ukahamisha kwa kutoa kadi na kuitunza nje ya simu (Njia hii haihitaji kuwa na kompyuta).

Kwa jinsi hii basi hutapata shida kwa kupoteza taarifa zako katika simu kwani utaweza ukarudisha taarifa zote pale unapopoteza simu na kununua simu mpya au pale unapobadirisha simu.
Unaweza ukafanya mwenyewe kama ni mjuzi wa kutumia simu na kompyuta, vinginevyo omba msaada wa kitaalamu toka kwa mtu anayefahamu. Wataalamu wa TEHAMA wanaweza kukupa msaada mzuri zaidi.
Kumbuka kuwa mbinu hizi ni baadhi ya simu tu ambazo zina uwezo mkubwa au “Smartphone”.

0 comments:

 

LIKE PAGE YETU UWE WA KWANZA KUPATA HABARI MPYA. Just Click Like Button Below...

Powered By OnlineBlogger