Baada ya danadana nyingi, Wananchi waamua kumwapisha Mwenyekiti wao wa Mtaa

Baada ya subira ya wiki mbili ili wenyeviti na wajumbe Mtaa wa Migombani – Segerea, Dar es Salaam waapishwe na mamlaka husika bila mafanikio, wananchi wameamua kuwaapisha viongozi hao kwa kutumia wakili binafsi.
 
Wakati hali hiyo ikitokea Dar es Salaam, wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro baadhi ya wenyeviti wa vijiji walioshindwa wamekataa kuwaachia ofisi viongozi wapya wakidai kuwa ofisi hizo ni mali ya CCM.
mkiti
 
Katika tukio la Segerea lilitokea jana asubuhi Segerea Mwisho, Japhet Kembo aliapishwa kuwa ‘mwenyekiti’ pamoja na ‘wajumbe’ watatu ambao ni Rose Bernard Mhagama, Nyangeto Justin na Ramadhan Seif wote wa Chadema bila kuishirikisha Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.
 
Akizungumza baada ya kuapishwa, Kembo alisema wananchi wamechoshwa na danadana wanazopigwa na Manispaa ya Ilala za kutowaapisha viongozi waliowachagua.
 
Wananchi wamemtafuta wakili ambaye amekuja kusimamia suala hili kisheria na ndiyo maana zoezi limefanywa hadharani,” alisema Kembo.
 
Kembo alisema katika nafasi ya uenyekiti alipata kura 547, Uyeka Idd wa CCM kura 273 na Erick Mchata wa NCCR-Mageuzi kura 205.

0 comments:

 

LIKE PAGE YETU UWE WA KWANZA KUPATA HABARI MPYA. Just Click Like Button Below...

Powered By OnlineBlogger