SHEHENA KUBWA YA SUKARI ILIYOIBIWA NA MAJAMBAZI HAPA BONGO YAKAMATWA...



Shehena ya sukari yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni tisini iliyoibiwa na majambazi kwa kutumia silaha na kuwakata mapanga kichwani baadhi ya walinzi katika moja ya ghala ya kuhifadhia bidhaa eneo la Mbagala rangi tatu jijini Dar es salaam zimekamatwa na jeshi la polisi huko Chamazi kabla ya kufikishwa sokoni kwa ajili ya kuuzwa.
Baada ya kupatikana kwa fununu ya kukamatwa kwa shehena ya mifuko mingi ya sukari, ITV ilitua katika ofisi za polisi wilaya ya Mbagala maarufu kwa jina la kituo cha Maturubahi ili kujionea ukweli, ambapo camera ya ITV ilishuhudia lori kubwa yenye namba za usajili T.524 AJZ aina ya scania ikiwa imepakia mifuko ya sukari ambazo tayari zilikuwa zimeibiwa usiku wa tarehe 4 mwezi August 2013.
Baada ya ITV kushuhudia mifuko 1312 za sukari, ambayo kila mfuko ina kilo hamsini, ITV ililazimika kufika eneo la Mbagala rangi tatu katika ghala ya bwana Haruni Zakaria mmiliki wa kampuni ya Al-Naiem Enterprises  ambapo sukari hiyo ilihifadhiwa na kukuta damu katika maeneo ambayo walinzi wa ghala hiyo walipigwa na kufungwa kamba kama  anavyoeleza kamanda wa mkoa wa Temeke ACP Englibert Kiondo.
Wakati tukio hilo linatokea baadhi ya majambazi hao walijitahidi kufanya kila waliwezalo ili kuzimisha sakata hilo,lakini maafisa wa jeshi la polisi waliamua kusimamia maadili yao ya kazi kwa kukataa rushwa  huku wakiwabana wahusika  hao kijeshi ili kutaja mtandao mzima wanaohusika  ambapo maafisa wa jeshi walifanikiwa kufika hadi Chamazi eneo linalotumika katika kuficha sukari kabla ya kusambaza sokoni.
Kutokana na tukio hilo kuleta hisia kwa wakazi wa maeneo hayo,licha ya watuhumiwa kumi na mbili kushikiliwa  na jeshi la polisi, lakini baadhi ya mashuhuda walilazimika kutoa maoni yao.

0 comments:

 

LIKE PAGE YETU UWE WA KWANZA KUPATA HABARI MPYA. Just Click Like Button Below...

Powered By OnlineBlogger