AZAM FOOTBALL CLUB

 

Azam F.C. Football club Azam Football Club is a Tanzanian football club who playing in the Tanzanian Premier League. It's a team that got promotion into the Premier League for the first time ever on the last season 2008/09.
 Founded: June 24, 2007
 League: Tanzanian Premier League


Azam FC yafanya kufuru Sudan Kusini, yaichakaza Al Nasri Juba 5-0



Ushindi wa 5-0 dhidi ya Al Nasri Juba ya Sudan Kusini, umeipa Azam FC nafasi ya kuingia hatua ya pili ya mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa kuitoa timu hiyo kwa jumla ya magoli 8-1.
Azam FC inashiriki kwa mara ya kwanza mashindano hayo yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) imefanikiwa kuvuka hatua ya awali na kuingia hatua ya pili ambapo zimesalia timu 36.
Azam FC imefikisha idadi hiyo ya magoli baada ya kupata ushindi wa 3-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wiki mbili zilizopita na leo wakacheza mechi ya pili kwenye Uwanja wa Juba nchini Sudan Kusini na kupata ushindi mnono wa 5-0 wakiwa ugenini na kufikisha jumla ya magoli 8-1.
Kwa timu za Tanzania zinazoshiriki mashindano ya CAF, ni Azam FC pekee iliyosalia baada ya timu za Simba SC kutolewa na Recreativo Libolo ya Angola kwa jumla ya magoli 5-0, na Jamhuri ya Pemba nayo ikatolewa na St. George ya Ethiopia kwa kipigo cha jumla cha 8-0 zote zilikuwa zinacheza Klabu Bingwa Afrika.
Azam FC wanabaki kuwa wawakilishi pekee wa Tanzania katika mashindano ya CAF, watakutana na mshindi kati ya Barrack Y. C. II ya Liberia na Johansens ya Sierra Leone.
Katika mchezo wa leo ambao Azam FC walipata ushindi wa 5-0, magoli yalifungwa na Khamis Mcha magoli matatu ‘Hat Trick’, John Bocco na Salum Abubakar wamefunga goli moja moja.
Azam Fc katika mchezo wake wa kwanza ilipata ushindi wa 3-1 magoli ya Azam FC yakifungwa na Abdi Kassim na Kipre Tchetche aliyefunga magoli mawili.
Kikosi kamili cha Azam Fc kitarejea nchini kesho kwa maandalizi ya mchezo wao mwingine wa Kombe la Shirikisho utakaochezwa kati ya Machi 15-17 mwaka huu.





Azam yaendeleza wimbi la ushindi Monrovia



 
Goli la mchezaji Abdalah Seif ‘Karihe’ wa Azam FC limepeperusha vyema bendera ya Tanzania baada ya kupelekea timu hiyo kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Baraack YC II katika mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika uliochezwa jana usiku kwenye Uwanja wa ATS jijini Monrovia nchini Liberia.
 
Wawakilishi hao pekee wa Tanzania katika mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrka (CAF)  wameshinda mchezo huo wa ugenini katika hatua ya pili ya mashindano hayo makubwa Afrika, mechi ya marejeano itachezwa wiki mbili zijazo jijini Dar es Salaam.
 
Azam FC wakiwa na kila aina ya sababu ya kushinda kutokana na maandalizi waliyofanya pamoja na mipango mizuri ya timu hiyo iliyowekeza katika soka wameweza kupambana na kupata matokeo hayo na kujiweka vizuri kwa ajili ya kuingia hatua nyingine ya mashindano hayo.
 
Katika mchezo huo Azam FC ilicheza ikimkosa mmoja wa manahodha wake Salum Abubakar ‘Sure Boy’ lakini timu ilicheza vizuri na kuwa na kasi zaidi, mchezaji Kipre Tchetche alikosa magoli mengi ya wazi katika kipindi cha kwanza.
 
BYC walikuwa wa kwanza kupata goli katika dakika ya 44 na kupeleka timu hiyo mapumziko wakiongoza 1-0 dhidi ya Azam FC.
 
Magoli yote ya Azam FC yalipatakana katika kipindi cha pili Humphrey Mieno aliweza kumchezesha kombolela kipa wa BYC na kufunga goli la kusawazisha dk 51 na kufanya matokeo kuwa 1-1.






Vodacom Premier LeagueStandings



tan

Rnk

Team
MP
W
D
L
GF
GA
+/-
Pts
1

Young Africans
20
15
3
2
37
12
25
48
2

Azam
19
11
4
4
32
16
16
37
3

Simba SC
19
9
7
3
28
16
12
34
4

Coastal Union
21
8
8
5
23
19
4
32
4

Mtibwa Sugar
21
8
8
5
23
19
4
32
6

Kagera Sugar
20
8
7
5
21
17
4
31
7

Ruvu Shooting
19
8
5
6
21
18
3
29
8

JKT Oljoro
21
6
7
8
20
23
-3
25
9

Mgambo JKT
21
7
3
11
15
21
-6
24
10

JKT Ruvu
20
6
4
10
19
32
-13
22
11

Tanzania Prisons
20
4
8
8
11
17
-6
20
12

Polisi Morogoro
21
3
8
10
12
22
-10
17
13

Toto African
21
3
8
10
17
29
-12
17
14
African Lyon
21
4
4
13
14
32
-18
16




tr>

AJABU KWELI

,

0 comments:

 

LIKE PAGE YETU UWE WA KWANZA KUPATA HABARI MPYA. Just Click Like Button Below...

Powered By OnlineBlogger